Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya Simba kufuzu, Manara atatimiza ahadi?

Jumapili , 17th Mar , 2019

Simba imeweka historia nyingine kwa Tanzania baada ya kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika jana katika Uwanja wa Taifa.

Kushoto, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Mohamed Dewji akishangilia ushindi wa Simba.

Kwenye mchezo huo wa mwisho wa hatua ya makundi dhidi ya AS Vita, Simba ilihitaji ushindi wowote ili ifuzu hatua ya robo fainali, jambo ambalo lilifanikiwa kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mabao yaliyofungwa na Mohamed Hussein katika dakika ya 36 na Clatous Chama katika dakika ya 90 huku bao pekee la AS Vita likifungwa na Kasendu Kazidi katika dakika ya 13.

Kabla ya mchezo huo, Afisa Habari wa Simba, Haji Manara aliahidi kupitia kipindi cha Kipenga Xtra cha East Africa Radio kuwa endapo klabu yake itaibuka na ushindi, hatowasema mahasimu wake Yanga kama alivyokuwa akifanya hapo awali, bali atakaa kimya.

"Mashabiki wa Yanga wananihofia sana mimi, wanaogopa kuisapoti Simba kisa eti mimi nitasemaje. Sasa naahidi Simba ikishinda sitowasema Yanga, nitaishia kusema tu 'Alhamdulillah'", alisema Manara, Ijumaa, Machi 15.

Lakini kinachoonekana hivi sasa baada ya ushindi huo ni muendelezo wa maneno yake ya utani kwa mahasimu wake ambao amesema walikuwa wakiidharau timu yake.

Ahadi nyingine ambayo aliihidi Manara ni kuwa endapo mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara watavuka hatua hii ya makundi na kwenda robo fainali, basi yatakapomalizika mashindano hayo mwezi June, yeye ataitwa Msemaji wa Mabingwa wa Afrika.

Simba imevunja rekodi yake yenyewe kuwa klabu ya kwanza Tanzania tangu mwaka 1974 kufuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Klabu Bingwa barani Afrika, ambapo sasa itaungana na timu za Waydad Casablanca, Mamelodi Sundowns, TP Mazembe, SC Constantine, Horoya, Esperance Tunis pamoja na Al Ahly.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi