Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Barcelona yaongoza duniani kwa wafuasi mtandaoni

Alhamisi , 23rd Jan , 2020

Mtandao unaojihusisha na masuala ya data na fursa za kimtandao kwa wanamichezo, vilabu na mashirikisho wa 'Result Sports' wenye makao makuu mjini Büdingen nchini Ujerumani umetoa listi ya klabu za soka zenye wafuasi wengi duniani katika mtandao ya kijamii.

Wachezaji wa Barcelona na Simba

Data hizo zilizotolewa mwezi Januari 2020 zinaonesha kuwa Barcelona inaongoza duniani kuwa na wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii, ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 260 kutoka katika mitandao yake ya Instagram, Twitter, Facebook, YouTube na milioni 8 kutoka mitandao mingine.

Real Madrid inakamata namba mbili ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 258, Manchester United ikishika namba tatu ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 142. Chelsea ina wafuasi zaidi ya milioni 93 katika nafasi ya nne huku Juventus ikishika namba tano kwa wafuasi zaidi ya miloni 90, nafasi ya sita ni Bayern Munich, Liverpool nafasi ya saba, PSG nafasi ya nane, Man City nafasi ya tisa na Arsenal nafasi ya 10.

Kwa klabu za Afrika, mabingwa mara nane wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika Al-Ahly inaongoza kwa wafuasi wengi ikiwa na zaidi ya wafuatiliaji milioni 25, ikishika namba 18 duniani. Nafasi ya pili kwa Afrika inafuatiwa na Zamalek iliyo na wafuasi zaidi ya milioni 11 huku ikishika nafasi ya 32 duniani.

Kwa Afrika Mashariki inaongozwa na klabu ya Simba ambayo imeingia kwa mara ya kwanza katika listi hiyo, ambayo imeshika nafasi ya 151 duniani huku ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni moja. Facabook ina wafuasi zaidi ya 568,000, Instagram ikiwa na wafuasi zaidi ya milioni 1, Twitter ina wafuasi takribani 142,000 na YouTube ikiwa na wafuasi zaidi ya 21,000.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya