Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bball Kings yapeleka nyota wa kikapu Canada

Alhamisi , 8th Nov , 2018

Mwanafunzi wa sekondari jijini Dar es salaam ambaye ni mchezaji wa timu ya taifa ya kikapu ya U18,  Atiki Ally Atiki amefanikiwa kupata udhamini wa Kwenda kusoma elimu ya juu ya sekondari nchini Canada kwenye shule ya Themes Valley district school Board.

Mchezaji wa kikapu, Atiki Ally Atiki

Atiki amepata udhamini huo kupitia taasisi ya JUCO Advocates ambayo ilikuja hapa nchini kwa mualiko wa kocha wa timu ya Taifa Matthew McAllister kupitia mafunzo maalumu yaliyoyafanyika mwezi Agosti 2017.

Atiki Anatarajiwa kuanza masomo Februari mwakani na katika kipindi kilichosalia kabla ya kujiunga na shule hiyo, atakua akifanya mazoezi na kucheza katika kituo cha, London Basketball Academy iliyopo katika mji wa Ontario, Canada. Anatarajiwa kumaliza masomo na kupata secondary school diploma mwezi wa tisa mwaka kesho. 

Safari ya Atiki katika Mpira wa kikapu ilianzia Mwanza miaka miwili iliyopita alipohamia Dar Es salaam na kusoma shule ya msingi Gerezani huku akifanya mazoezi katika timu ya JMK PARK Academy. Amecheza kwa Muda Mfupi kwenye timu ya Jogoo na baadae kupandishwa kucheza kwenye timu ya Kwanza ya Vijana baada ya kufanya vizuri.

Atiki ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Vijana U18 ambapo mwaka huu alishriki kwenye mashindano ya zone 5 na akachaguliwa kuwa miongoni mwa wachezaji 5 bora katika shindano hilo.

Pia alishiriki katika michuno ya kikapu ya Sprite Bball Kings iliyofanyika mwezi Juni na Julai mwaka huu inayoandaliwa na EATV, ambapo alikuwa mchezaji wa Portland.
Katika michuano hiyo, Portland ilifanikiwa kucheza hatua ya fainali dhidi ya Mchenga Bball Stars ambapo Portland ilifungwa katika michezo yote mitatu.

London Basketball Academy ambayo Atiki atajiunga nayo, inashiriki kwenye mashindano mbalimbali nchini Canada na Marekani.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali