Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Bball Kings itawapeleka watu kimataifa' - Mohamed

Ijumaa , 3rd Aug , 2018

Nahodha wa Mchenga Bball Stars, Mohamed Yusuf, amefunguka kuwa ukubwa wa michuano ya Sprite Bball Kings inayoandaliwa na East Africa Television LTD na kudhaminiwa na kinywaji cha Sprite, unatosha kuwapa nafasi wachezaji ya kuonekana na pengine kucheza kimataifa. 

Mohamed Yusuf katikati akijadili jambo na wenzake wakati wa mchezo wao dhidi ya Portland.

Mohamed Yusuf ameyasema hayo kwenye mahojiano maalum na kipindi cha East Africa Breakfast kupitia East Africa Radio, ambapo ameeleza kuwa mbali na zawadi wanazopata washindi lakini ukubwa wa michuano hiyo ndio kitu kingine kinachowafanya wajitume zaidi.

''Unajua kwenye michuano hii kila mchezaji anajitahidi kuonesha kiwango chake sio tu kwaajili ya kupata zawadi bali kutokana na ukubwa wa michuano hii watu wanawaza kupata nafasi ya kucheza kimataifa na ninaamini jambo hilo linawezekana'', - amesema.

Mbali na hilo Mohamed maarufu kama Mood, ameongelea 'game 2' ya nusu fainali ambapo amesema wanatarajia kukata tiketi ya fainali kesho akidai haoni kama wapinzani wao ambao ni Portland watawazuia haswa baada ya kushinda game 1 kwa pointi 70 dhidi ya 54.

Game 2 za best of three ya nusu fainali ya Sprite Bball Kings zitapigwa kesho Jumamosi Agosti 4 kwenye uwanja wa taifa wa ndani jijini Dar es salaam. Flying Dribblers baada ya kushinda 'game 1' kwa pointi 84 kwa 75 za Team Kiza watakipiga tena kutafuta nafasi ya fainali. Mchenga nao watakipiga na Potrland. Mechi zitaanza saa 10:00 jioni na hakutakuwa na kiingilio.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa