Alhamisi , 10th Jan , 2019

Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa klabu ya Yanga, Dr. Jonas Tiboroa amejinasibu kurejesha mfumo wa zamani wa klabu hiyo ambao utaruhusu klabu kuwa na kampuni mbili za kibiashara.

Dr. Jonas Tiboroa na Yusuph Manji

Katika muendelzo wa kampeni zake kuelekea uchaguzi huo, Dr. Tiboroa amesisitiza kuwa klabu ya Yanga itaendelea kuwa ya wanachama huku kukiwa na kampuni mbili, kampuni moja itakuwa inahusika katika uwekezaji na nyingine ambayo itahusika na biashara za klabu.

"Mimi nilipokuwa Katibu Mkuu chini ya Manji tulisema tutahakikisha kuwa Yanga inakuwa klabu ya wanachama na tukaanzisha kampuni mbili, moja inayoshughulikia uwekezaji na nyingine inayoshughulikia biashara za klabu", amesema.

"Hizi kampunni tulizisajili mwaka 2015, lakini kwa bahati mbaya kizo kampuni zote hazijafanya kazi mpaka sasa, ndiyo maana mimi nimeona kuna haja ya kurudi nikaendeleze yale niliyoyaanza", ameongeza Dr. Tiboroa.

Endapo Dr. Tiboroa atachaguliwa na mpango huo kukamilika, maana yake wawekezaji kama Yusuph Manji na wengine wanaweza kupata nafasi ya nafasi ya kuwekeza katika klabu hiyo bila kuathiri mfumo wake wa uanachama kwakuwa shughuli zote zitaratibiwa chini ya kampuni ya uwekezaji ya klabu.

Uchaguzi wa Yanga unatarajia kufanyika Januari 13, 2019 kwenye ukumbi wa bwalo la maafisa wa polisi Oysterbay Dar es salaa, ambapo nafasi ya Uenyekiti wa klabu inashindaniwa na wagombea  wawili, Dr. Jonas Tiboroa na Baraka Igangula.