Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Firmino kama Kagere au Kagere kama Firmino?

Jumatano , 19th Sep , 2018

Gumzo kubwa katika mchezo wa jana wa Liverpool na PSG ni katika staili ya ushangiliaji ya mshambuliaji wa Liverpool, Roberto Firmino baada ya kufunga bao la tatu na la ushindi katika dakika za majeruhi.

Pichani, mshambuliaji wa Liverpool, Roberto Firmino (kushoto) na mshambuliaji wa klabu ya Simba, Meddie Kagere.

Firmino alishangilia kwa staili ya kuziba jicho moja, staili ambayo kwa mashabiki wa soka nchini Tanzania na hata Afrika Mashariki wanaishuhudia kwa mshambuliaji wa klabu ya Simba, Meddie Kagere ambaye anashangilia kwa staili ya kuziba jicho moja kila anapofunga bao.

Kagere amekuwa akiitumia staili hiyo tangu akiwa katika klabu ya Gor Mahia ya Kenya na hata anapofunga bao katika timu yake ya taifa ya Rwanda.

Mashabiki na wadau wa soka wamekuwa wakikinzana juu ya nani mwanzilishi wa staili hiyo au nani ambaye ameipa umaarufu kiasi cha kujukikana kwa kiasi hicho. Wapo wanaosema kuwa Kagere ndiye anastahili kuitwa mwanzilishi wa staili hiyo au aliyeipa umaarufu huku wengine wakisema kuwa mshambuliaji huyo wa Simba ameiga staili hiyo kutoka Ulaya ambako wachezaji wengi wamekuwa wakiitumia na hastahili kuwa ndiye mchezaji aliyeipa umaarufu.

Kwa upande wa Roberto Firmino, yeye amekuwa ni mchezaji mwenye staili nyingi za ushangiliaji, misimu miwili iliyopita aliwahi kuwa na staili maarufu ya ushangiliaji ya kuvua shati anapofunga kabla ya kuiacha kutokana na kuadhibiwa kwa kadi za njano mara nyingi alipokuwa akifanya hivyo.

Pia aliwahi kuwa na staili maarufu ya ushangiliaji ya ‘Samba dance’ aliokuwa akicheza na Mbrazil mwenzake Phillipe Coutinho aliyetimkia Barcelona. Staili hizo  zimekuwa zikitumiwa na wachezaji wengi wa Brazil ambazo zinatokana na ngoma maarufu nchini kwao ya ‘Samba’.

Mwisho wa siku ukweli haujajulikani kuwa ni nani hasa mwanzilishi au mchezaji aliyeipa umaarufu staili hiyo kiasi cha kummilikisha kuwa ni yake kama ilivyo staili maarufu ya ushangiliaji ya Cristiano Ronaldo, ambayo aliitumia pia katika bao lake la kwanza kwenye mchezo wa Serie A wikiendi iliyopita dhidi ya Sassuolo.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa