Jumatano , 14th Mei , 2025

Indiana pacers  imekua timu ya kwanza kutinga fainali ya NBA kutoka ukanda  wa Mashariki  baada ya kupata ushindi wa vikapu 114- 105 dhidi ya Cleveland cavaliers 

Indiana Pacers

Kwenye michezo yao mitano Indiana pacers wameshinda michezo  minne ambapo kwa sasa wanasubiri mshindi kati ya Boston Celtics na New York Knicks ambao watashuka dimbani usiku wa leo Mei 14 2025

Mchezaji bora wa mchezo  huo ni Tyrese Haliburton amefunga points 31 ,Rebound 6,Assist 8

Mchezo mwingine uliopigwa usiku wa jana ni Oklahoma City Thunder wameitandika Denver Nuggets vikapu 112-105 huku Shai Gilgeous-Alexander akifunga pointi 31 zilizowapeleka  mbele kwa mabao 3-2 katika mfululizo wao wa nusu fainali ya kanda  ya Magharibi.

Huku nyota wa  Nuggets Nikola Jokic alifunga   points 44 na rebounds 15, lakini hakuweza kuwazuia Oklahoma City kuibuka  washindi  katika mchezo wao wa tano wa playoff.