Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ivo Mapunda na Taulo lake kurejea ligi kuu Kenya

Jumamosi , 9th Jul , 2016

Baada ya kutokuwa na misimu kadhaa yenye mafanikio akichezea vilabu vya Simba SC na Azam FC za Tanzania kipa maarufu nchini ambaye aliwahi kudakia timu ya Yanga SC Ivo Mapunda huenda akarejea nchini Kenya ambako alipata umaarufu akiwa na Gor Mahia

Kipa Ivo Mapunda wakati huo akiichezea Simba SC ya Dar es Salaam Tanzania.

Kipa Ivo Philip Mapunda aliyemaliza mkataba wake katika klabu ya Azam FC amesema anaimani rekodi aliyoiacha nchini Kenya misimu kadhaa takribani miaka mitatu iliyopita akiwa na mabingwa wa nchi hiyo Gor Mahia maarufu kama Ingwe itambeba katika harakati zake za kusaka maisha mapya katika soka nchini humo.

Ivo ameanza mikakati mizito ya chinichini ili kurejea nchini humo ambako alipata umaarufu mkubwa akidaka huku akiwa na taulo kubwa golini baada ya kumaliza mkataba wake na Azam FC waliomsajili kutoka klabu ya Simba na klabu hiyo kutangaza kutomwongezea mkataba mpya huku ikishusha makipa wawili wakimataifa toka Hispania na Ivory Coast ambao tayari wameanza majaribio na timu hiyo katika viwanja vya Chamazi jijini Dar es Salaam.

Aidha Mapunda mzaliwa wa jiji la Mbeya mwenye asili ya Songea ambaye kabla ya kutua Gor Mahia alianza maisha ya soka nchini Kenya akiwa na klabu ya Bandari ya Mombasa aliyojiunga nayo akitokea kwa mabingwa wa Tanzania Yanga SC amesema mipango yake ya kwanza ni kurejea kucheza ligi kuu ya Kenya ambayo kwa sasa bado inaendelea ila kwa kipindi hiki anataraji kujisajili kwa timu ambayo itampa kandarasi [mkataba] ya muda mfupi.

Akimalizia Mapunda amesema yeye bado anauwezo mkubwa kama awali na umeongezeka mara dufu na kimsingi kuwekwa benchi katika klabu ya Azam si kwamba uwezo wake ulikuwa mdogo ila ni mipango ya kocha wa timu hiyo kuamua mtumia zaidi kipa kinda mwenye kipaji kikubwa Aishi Manula na yeye na mwenzake Mwadini Ally kubadilishana benchi wakati kinda huyo aliyeibukia katika michuano ya Uhai Cup akitamba mpaka katika timu ya taifa Stars.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi