Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kamusoko afunguka kinachoitesa Yanga

Jumanne , 22nd Mei , 2018

Nyota wa Klabu ya Yanga na wawakilishi pekee Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa, Thaban Kamusoko amefunguka na kudai sababu kubwa iliyowasababisha kufanya vibaya katika michezo yao Ligi ni kutokana na kubanwa na ratiba japo ambalo lilipelekea kushindwa kupata muda mzuri wa kujiandaa.

Kamusoko ametoa kauli hiyo jioni ya leo Mei 22, 2018 muda mchache ilipomaliza mechi yao dhidi ya Mbao FC ambapo Yanga imefanikiwa kutoka na ushindi wa bao 1-0 lililopachikwa na mchezaji huyo na kuifanya timu yake kupata matokeo mazuri baada ya kupitia msoto mkali wa vipigo vitano na sare nne kwenye mechi zilizopita katika mashindano yote ya ligi kuu.

"Cha kwanza namshukuru Mungu tumepata ushindi, katika mchezo wa leo kitu ambacho tulikuwa tumejiwekea akilini ni kupata ushindi kwasababu Yanga ukiangalia ni timu kubwa yenye watu wengi kwa hiyo inahitaji ushindi kwa kila mechi", amesema Kamusoko.

Aidha, Kamusoko amesema sababu kubwa ya Yanga kufanya vibaya katika michezo yake ya hivi karibuni ni kutokana na kubanwa na ratiba ambayo iliwapelekea kushindwa kupumzika vizuri ili wapate kujiandaa na michezo iliyokuwa inawakabiri.

Pamoja na hayo, Kamusoko amesema watajitahidi kufanya vizuri katika michezo yao miwili iliyosalia ili waweze kujikunyakulia alama 6 ambazo zitawaweza kuwaweka sehemu nzuri kwenye msimamo wa ligi Kuu Tanzania Bara.

Kwa ushindi wa leo, Yanga imeweza kufikisha alama 51 kwenye mechi 29 na kuendelea kuwa katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam FC yenye alama 55 na Simba yenye alama 68 kileleni.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali