Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Klopp aomba msamaha kiaina Camp Nou

Jumatano , 1st Mei , 2019

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp ameonesha kutofurahishwa na namna waandishi wa habari walivyomnukuu juu ya kauli yake kuhusu uwanja wa Barcelona, Camp Nou.

Kocha Jurgen Klopp

Klopp amesema kuwa wanahabari wameandika habari potofu juu ya kauli yake aliyozungumzia uwanja wa Camp Nou, alipoulizwa maoni yake kufuatia kurasa za mitandao ya kijamii za Barcelona kupost video iliyoambatana na maneno, "nyumbani kwetu, hekalu letu, ngome yetu".

Akizungumza katika mkutano na wanahabari kuelekea mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Klabu Bingwa Ulaya kati ya FC Barcelona na Liverpool katika dimba la Camp Nou, usiku wa leo, Klopp amesema, "haikuwa ni kwaajili ya kudharau kwasababu Barcelona walikuwa wakitawala, ilikuwa ni muhimu kwa timu kufahamu kuwa ilikuwa ni uwanja wa kawaida na sio hekalu, ngome au kitu kingine", amesema.

"Ninaongea vitu 500,000 vya msingi kuhusu Barcelona, mnajaribu kucheza mchezo kwa kubadilisha maneno na kuyafanya mambo kuwa makubwa, mimi ni shabiki wa soka kwa muda mrefu kuliko hata kazi yangu ya ukocha, mnafikiri nitasema nini kibaya kuhusu uwanja huu?".

Barcelona itakutana na Liverpool usiku wa leo, huku Liverpool ikiwa na rekodi nzuri ya kutopoteza mechi nne za ugenini dhidi ya Barcelona, ikishinda mechi mbili na kutoka sare mechi mbili. Barcelona pia imeshinda mechi nyingi zaidi (27) dhidi ya timu za Uingereza, kuliko timu nyingine yoyote ya nje ya Uingereza katika michuano ya Ulaya.

Pia akimzungumzia kiungo wa Barcelona, Phillipe Coutinho, kocha Jurgen Klopp amesema kuwa alipenda kufanya kazi na mchezaji huyo kwa saababu ni mchezaji bora wa kiwango cha Dunia na aliposikia kwa mara ya kwanza kuwa anataka kwenda Barcelona alikuwa akiwaza timu yake ambavyo itacheza bila ya uwepo wake.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa