Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

KMC yawajibu Stand United

Jumatano , 11th Jul , 2018

Klabu ya manispaa ya Kinondoni (KMC), imejibu tuhuma dhidi yao ya kumsajili mchezaji Ally Ally kutoka Stand United wakati akiwa na mkataba wa miaka miwili na klabu yake.

KMC kupitia kwa mkurugenzi wake, Walter Urio imesema kuwa wamemsajili Ally Ally baada ya kujiridhisha kuwa yuko huru, alipovunja mkataba na klabu yake na ushahidi wanao huku wakiitaka Stand United ilete ushahidi wao mezani watawajibu.

“Sisi tumemsajili Ally Ally baada ya kujiridhisha kuwa yuko huru, alivunja mkataba na Stand United baada ya kudai malimbikizo ya mshahara wake wa miezi minne na ushahidi wa nakala ya barua ya kuvunja mkataba ipo SPUTANZA na TFF kwahiyo wao kama bado wanadai ni mchezaji wao basi wapeleke ushahidi TFF “. Amesema Urio.

Stand United kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili, Mbasha Matutu ulionesha kusikitishwa juu ya usajili huo kwani hawakuwa na taarifa yoyote juu ya kuondoka kwake Shinyanga kuja Dar es salaam na kusaini KMC.

Matutu pia amekana tuhuma za kushindwa kumlipa mshahara wa miezi minne mchezaji huyo kuwa ni sababu iliyopelekea kuvunja mkataba naye huku akisisitiza kuwa wao walikuwa wakimlipa mshahara wake kila mwezi kama kawaida na hawana deni lolote kwake.

Ally Ally amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya KMC ambayo imepanda kucheza ligi kuu Tanzania Bara kuanzia msimu ujao wa 2018/19.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke