Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kocha Serengeti Boys agoma kuachia ngazi

Alhamisi , 18th Apr , 2019

Baada ya kupoteza mchezo wa pili mfululizo wa michuano ya vijana chini ya miaka 17 ya AFCON inayoendelea nchini, kocha wa Serengeti Boys, Oscar Mirambo amesema haoni sababu ya kung'atuka katika timu hiyo.

Kocha wa Serengeti Boys, Oscar Mirambo

Jana, April 17, Serengeti Boys imepoteza mchezo wa pili mfululizo dhidi ya Uganda na kupelekea kufifisha matumaini ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia ya Vijana chini ya miaka 17, itakayofanyika nchini Brazil.

Mirambo amesema kuwa haoni sababu ya kung'atuka kuifundisha Serengeti Boys kwasababu vijana hao wamewekewa mipango ya kukuzwa na itaendelea kama kawaida kwa mashindano yajayo.

"Kuhusu kama nimeshindwa kuipeleka timu katika fainali za Kombe la Dunia niachie nafasi hii sidhani kama litakuwa jambo sahihi kwa maana nitakuwa nakimbia changamoto. Timu ina mipango na mashindano yanaendelea, ninaweza kuamua kung'atuka lakini ni kwa mustakabali wa nani," alisema Mirambo.

Serengeti walifungwa mechi ya kwanza na Nigeria kwa mabao 5-4, na katika mchezo dhidi ya Uganda wakakubali tena kichapo cha mabao 3-0, ambapo sasa inasubiri kumalizia mchezo wa mwisho katika kundi lao dhidi ya Angola.

Mpaka sasa timu zilizojihakikishia nafasi ya kufuzu Kombe la Dunia la vijana ni timu za vijana za Cameroon na Nigeria.
 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa