Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mabondia wawili wafariki kwa kupigwa ulingoni

Ijumaa , 26th Jul , 2019

Mchezo wa ngumi ni miongoni mwa michezo inayopendwa zaidi duniani, haswa kutokana namna inavyoweza kutengeneza majina makubwa kama ilivyowahi kuwa kwa mabondia Muhammad Ali na Mike Tyson ambao walijijengea heshima duniani kote.

Kushoto ni bondia Maxim Dadashev na kulia ni bondia Hugo Santillan.

Wiki hii imekuwa si nzuri kwa mchezo huo kutokana na mabondia wawili kupoteza maisha baada ya kuumia wakiwa ulingoni.

Bondia Maxim Dadashev mwenye miaka 28, raia wa Urusi amefariki Jumanne Julai 23, 2019, ikiwa ni siku 4 zimepita baada ya kutoka ulingoni alikokuwa akipigana na Subriel Matias kwenye pambano la (IBF) Junior welterweight Ijumaa Julai 19 huko Maryland.

Kuna video zinaonesha jinsi mkufunzi wa Dadashev akimsisitiza bondia huyo wasitishe pambano kwani alikuwa na hali mbaya ikiwemo mwili kuchemka kupita kiasi.

Imeelezwa kuwa Dadashev alikuwa na tatizo kwenye ubongo lililotokana na kupigwa ngumi katika mapambano yake mbalimbali yaliyopita pamoja na hilo la Ijumaa.

Bondia mwingine ambaye amefariki wiki hii ni Hugo Santillan mwenye miaka 23 raia wa Argentina, ambaye amefariki baada ya kupigwa na kupoteza fahamu katika pambano dhidi ya Eduardo Abreu wa Uruguay.

Santillan alikimbizwa hospitali na kufanyiwa upasuaji wa ubongo na kinga ya mwili lakini amefariki siku 5 baada ya pambano hilo.

Santillan na Eduardo Javier  walipigana Jumatano usiku huko Buenos Aires Argentina, kwenye pambano la Super lightweight.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali