Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makambo azungumzia kuchukua uraia wa Tanzania

Ijumaa , 12th Apr , 2019

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya DR Congo, Heritier Makambo amefunguka juu ya uwezekano wa kuchezea timu ya taifa ya Tanzania endapo ataombwa kubadili uraia.

Heritier Makambo

Amezungumza hayo baada ya mchezo wa Ligi Kuu kati ya Yanga na Kagera Sugar katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza, ambao Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-2.

Makambo amesema kuwa hafikirii kwa sasa kubadili uraia ili kuichezea Tanzania na hata kama ikimuhitaji hatoweza kwa sababu anajivunia na taifa lake.

"Kwangu ni furaha kuitwa katika timu ya wachezaji 40 ya taifa, hata kama nisipopata nafasi ya kucheza lakini kwangu ni kama ndoto na heshima kuwepo", amesema Makambo.

Pia akizungumzia juu ya moto wake wa kufunga katika dimba la CCM Kirumba, ambapo mpaka sasa amefanikiwa kufunga mabao matano, manne yakiwa ni ya ligi na bao moja la kombe la shirikisho, Makambo amesema,

"Kitu kinachochangia zaidi ni uzuri wa uwanja wa CCM Kirumba, unafanana na uwanja wa Taifa. Lakini pia kufunga kwangu kunaletwa na juhudi zinazofanywa na wachezaji wote wa Yanga, tunasaidiana sana ndiyo maana naweza kufunga", ameongeza.

Rekodi ya Makambo CCM Kirumba

 

Baada ya kufunga bao katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar, Makambo amefikisha jumla ya mabao 15 ya Ligi Kuu, akimfukuzia mshambuliaji wa Mwadui FC, Salim Aiyee ambaye amefunga mabao 16.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa