Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara amtaka Mwinyi Zahera kujifunza

Jumapili , 21st Apr , 2019

Kufuatia kufungwa dhidi ya Kagera Sugar katika ligi, Afisa Habari wa Simba, Haji Manara amemtaka kocha wa Yanga kujifunza jinsi ya kuzungumza pindi timu yake inapofungwa.

Haji Manara na Mwinyi Zahera

Kupitia ukurasa wake wa Istagram, Manara ameanza kwa kumsifia kocha wake, Patrick Aussems kwa kitendo cha kuwapongeza wapinzani wake Kagera Sugar kutokana na kiwango walichokionesha dhidi yao, huku akimtaka kocha wa Yanga Mwinyi Zahera kuiga mfano huo badala ya kulalamika kuwa wanaonewa.

Manara ameandika, "tofauti ya kocha wa mpira na kocha wa Sunsumia au kibao kata!!. Unafungwa unawapongeza washindi na kukubali mapungufu yako, angekuwa yeye sasa!, "waamuzi wanatuonea, mimi nimefundisha Ulaya miaka arobaini", ( ukigoogle ) huoni timu alizofundisha zaidi ya kufundisha kucheza ndombolo na mayenu ). "Ohh Simba inabebwa, leo sikushinda kisa Ajibu na Fei Toto hawakuvaa boksa na hawajala toka juzi!!".

"Hahahahaha ila akishinda sasa, najua kupiga gitaa kuliko Diblo, na ile fasi ya putuluu imekuja na ndege na ndio maana sisi Wakongo tunapendwa na wadada wa bongo. Kocha mzuri huzungumzia vitu 'technical' na sio riwaya za wanaotumia mkorogo wa buku buku!!!", ameongeza Manara.

Baada ya kupoteza mchezo huo, sasa Simba inasalia na pointi zake 60 baada ya kucheza michezo 24, huku Kagera Sugar ikiwa katika nafasi ya 13 na pointi 39 baada ya kucheza mechi 33 mpaka sasa. 

Baada ya mchezo huo, Simba inaendelea na ratiba ya kupunguza viporo vyake ambapo sasa inajiandaa kucheza na Alliance FC jijini Mwanza, April 23 katika dimba la CCM Kirumba.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi