Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara amvaa tena Nugaz, ni kuhusu lugha

Ijumaa , 17th Jan , 2020

Mnyukano wa maneno unaendelea kati ya Afisa Habari wa Simba, Haji Manara na Afisa Mhamasishaji na Msemaji wa Yanga, Antonio Nugaz huku kila mmoja akijaribu kuisimamisha timu yake.

Haji Manara na Antonio Nugaz

Hali hiyo imekuwa ikionekana katika mitandao ya kijamii na hata katika mahojiano yao mbalimbali na vyombo vya habari, na kuleta mijadala mbalimbali miongoni mwa mashabiki wa timu hizo.

Hivi karibuni baada ya kumalizika kwa mchezo wa Yanga na Kagera Sugar na kushuhudia Yanga ikifungwa 3-0 nyumbani, Antonio Nugaz alikaririwa akisema kuwa walishindwa wenyewe kutumia nafasi walizozitengeneza, ambapo hii leo Haji Manara ameibuka na kukosoa lugha aliyotumia katika maelezo yake.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Manara amezungumzia kauli ya Nugaz kwa utani akisema, "rafiki yangu mimi huyo, eti ku'compose', najua alikusudia ku'convert', sitachoka kumweka sawa, mzigo wangu mwenyewe huu, halafu sasa hivi nishaanza kumfundisha kuongea kwa authority, sio hyo staili yake, huku kwenye soka ukiongea Mwamba wa Pua unaukaza kidogo, hii yaani huku sio, watu wa huku hovyo kidogo".

Tambo za maafisa hao zimeanza kuelekea kwenye mchezo wao uliopigwa wiki mbili zilizopita ambao ulimalizika kwa sare ya mabao 2-2, huku ushujaa ukionekana kwa Yanga ambao waliamka na kusawazisha mabao yote mawili ndani ya dakika 10 za kipindi cha pili cha mchezo.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke