Haji Manara
Manara amesema kuwa Simba ilistahili kushinda mchezo huo kutokana na uwekezaji ambao umefanywa mpaka sasa, huku akiwarushia lawama baadhi ya wachezaji kwa kutocheza kama mashabiki walivyotegemea.
Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 2-2, Simba ikitawala kwa kipindi cha kwanza ambapo ilipata bao moja, huku Yanga ikiamka na kushambulia kwa nguvu katikati ya kipindi cha pili na kufanikiwa kurejesha mabao yote mawili.
Sare hiyo imeonekana kufurahiwa na mashabiki wa Yanga huku wengi wakisema kuwa Simba walikwenda uwanjani na matokeo yao, hivyo wanafurahia kwa sababu walijihisi wanyonge kabla ya mchezo.