Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara azitaka pointi 6 za Mwanza, Mbao FC wajibu

Jumatano , 15th Jan , 2020

Kuelekea mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania Bara kesho Alhamis 16, 2020, klabu ya soka ya Mbao FC imesema imejiandaa vizuri licha ya wapinzani wao Simba kuwa na kila kitu kinachoweza kuwapa ushindi.

Kushoto ni Haji Manara na kulia ni wachezaji wa Mbao FC

Akiongea na EATV & EA Radio Digital, kocha msaidizi wa Mbao FC Abdulmutik Hajji ameweka wazi kuwa wamefanya maandalizi yao vizuri kwa kuzingatia ubora wa wapinzani wao.

'Tumejiandaa vizuri kuelekea mchezo wa ligi kuu kesho dhidi ya Simba lakini tunaiheshimu Simba kutokana na uzoefu mkubwa ilionao', amesema Hajji.

Kwa upande wa msemaji wa Simba Haji Manara amesema wanataka kupata pointi zote 6 za michezo miwili ya Mwanza ambayo ni dhidi ya Mbao FC na Alliance FC.

'Sasa akili yetu tuelekeze Mwanza katika mechi mbili ngumu zijazo, tushirikiane kupata pointi sita za CCM Kirumba, Insha'Allah tutafanikiwa', ameandika Manara.

Msimu huu Mbao FC wamecheza mechi 16 ambapo wameshinda mechi 4, Sare 6 na kufungwa mechi 6, wakati Simba wamecheza mechi 14, wameshinda 11, sare 2 na kufungwa 1.

Katika dirisha dogo la usajili Mbao FC wamesajili wachezaji watatu ambao Omary Wayne kutoka Ndanda SC walinzi Hussein Iddi kutoka Mtibwa Sugar na Mackyada Franco kutoka Coastal Union.

Simba wao wamesajili mchezaji mmoja ambaye ni Luis Miquissone kutoka UD Songo ya Msumbiji.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa