Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maneno ya kocha wa Uganda kwa Taifa Stars

Jumapili , 24th Mar , 2019

Kocha wa timu ya taifa ya Uganda, Sébastien Desabre amezungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi dhidi ya Taifa Stars, saa 12 jioni katika uwanja wa taifa.

Kocha wa Uganda, Sebastian Desabre (kushoto) na kikosi cha Taifa Stars.

Akizungumza katika mkutano na wanahabari kuelekea mchezo huo, Desabre amesema kuwa anajua kuwa wao wameshafuzu michuano ya AFCON na wanachotakiwa ni kuendeleza hatua hiyo.

"Maendeleo ya timu yetu katika hatua zinazofuata ni mazuri, tumekuwa ni miongoni mwa timu za kwanza kufuzu na kesho tutakuwa tunaendeleza maandalizi yetu ya hatua inayofuata ya AFCON", amesema kocha Desabre.

"Tanzania ina timu nzuri na kocha mzuri pia, tumeiona hata katika mchezo tuliocheza nao nyumbani. Najua kuwa wako katika 'pressure' kubwa ya kufuzu na kwa upande wetu tuna pressure ndogo lakini huu ni mchezo wa kimataifa, tutaonesha ushindani hata kama mchezo hautakuwa na faida sana kwetu", ameongeza.

Moja ya mechi kati ya Uganda Cranes na Taifa Stars

Kwa upande wake nahodha wa timu ya taifa ya Uganda, Denis Onyango amesema kuwa mchezo dhidi ya Taifa Stars kwao una umuhimu mkubwa huku akiita ni 'Derby' ya Afrika Mashariki.

"Tunajiandaa na michuano ya AFCON, mchezo wa kesho (leo) utakuwa ni wa kuvutia sana, itakuwa ni Derby ya Afrika Mashariki. Kama ilivyo kwao wanahitaji ushindi na sisi pia tunahitaji kushinda kwahiyo utakuwa ni mchezo mzuri kwetu kwaajili ya maandalizi kuelekea michuano hiyo", amesema Onyango.

Taifa Stars inahitaji ushindi ili iweze kufuzu wakati huohuo ikiiombea matokeo mazuri Cape Verde kwenye mchezo wake dhidi ya Lesotho.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa