Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Marufuku shindano  lolote la Tennis nchini China  

Alhamisi , 2nd Dec , 2021

Chama cha mchezo wa tennis duniani upande wa wanawake wamezuia mashindano yote yaliyopaswa kufanyika nchini China mpaka sakata la unyanyasaji wa kijinsia la nyota kutoka   nchini humo  Peng Shuai kupatiwa ufumbuzi.

(Mcheza tennis wa China, Peng Shuai na ujumbe alioutuma online)

Peng 35, aliyewahi kushika nafasi ya kwanza kwa ubora duniani kwa wachezaji wawili wawili kwenye tennis hakuonekana hadharani kwa siku 13 baada ya kuchapisha maneno kwenye mitandao yake ya kijamii mnamo November 2, 2021 kwamba aliyekuwa Waziri mkuu msaidizi nchini humo Zhang Gaoli alikuwa anamlazimisha kimapenzi kipindi alipokuwa hayupo kwenye mahusiano

Chapisho hilo lilikuja kufutwa saa chache baadae ingawaje tayari watu wengi walikuwa wamelisambaza na wasiwasi zaidi ukiongezeka kwa kutoonekana hadharani majuma mawili kwa nyota huyo

Mtendaji mkuu wa WTA, Steve Simon amesema “Bado tuna mashaka na usalama wa Peng, kama yupo huru, salama na kama hajatishiwa usalama wake” na kuendelea kusisitiza “kwa mazingira mazuri ya kiusalama , sidhani kama ninaweza kuwaambia wachezaji waende wakashindane huko”

 WTA kimetoa wito wa kuchunguzwa madai ya Peng huku wakisisitiza lazima ufanyike uchunguzi wa kina tena ulio wazi na huru bila ya kuwepo kwa vitisho.

Mara ya mwisho kuonekana kwa Peng ilikuwa mwisho wa mwezi Novemba 2021 kwenye michuano ya Beijing ya tennis kisha baadae kipande cha video kurushwa mtandaoni akiongea na rais wa kamati ya olimpiki (IOC) Thomas Bach na kusema yupo salama na mzima.

 Mamlaka za China zimesema suala la Peng  ni siasa za kimichezo tu.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya