Jumamosi , 27th Jun , 2020

Mashabiki wa soka wameruhusiwa kuhudhuria mchezo wa ligi kati ya Tanzania Prisons na Simba SC utakaochezwa kesho katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.

Mechi ya Mbeya City na Simba

Hiyo ni baada ya Serikali ya mkoa wa Mbeya kueleza mpango mkakati wa kusimamia kikamilifu mwongozo wa afya michezoni kwa Wizara yenye dhamana ya michezo nchini.

Katika taarifa yake iliyotolewa hii leo, Wizara imesema kuwa iwapo kutakuwa na uvunjifu wowote wa taratibu, hatua kali zaidi zitachukuliwa.

Soma zaidi taarifa kamili hapa.