Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mashali na Mwamakula kuwakilisha Taifa Venezuela

Jumanne , 28th Jun , 2016

Sasa ni rasmi mabondia wawili wa ngumi za kulipwa nchini waliojitokeza kuungana na ngumi za ridhaa kwa ajili ya Olimpiki ndiyo wataiwakilisha nchini katika michuano ya kuwania tiketi ya kushiriki michuano ya Olimpiki huko Venezuela.

Bondia Thomas Mashali.

Shirikisho la Ngumi nchini Tanzania BFT limesema mabondia wawili wa ngumi za kulipwa Amos Mwamakula na Thomas Mashali walioingia katika ngumi za ridhaa ili kushiriki michuano Olimpiki ndiyo wataelekea nchini Venezuela.

Rais wa BFT Muta Rwakatale amesema mabondia hao wote wako vizuri na tayari taratibu zao za safari kuelekea nchini Venezuela zimekamilika.

Muta ambaye ni bondia wa wazamani wa ngumi za ridhaa amesema baada ya kupata maombi ya nia thabiti ya mabondia hao kuonyesha uzalendo yakutaka kuiwakilisha nchi katika michuano hiyo mikubwa wao kama shirikisho BFT na kwakufuta agizo la chama cha kimataifa cha ngumi duniani AIBA kupitisha sheria ya mabondia wa kulipwa kuingia ngumi za ridhaa yaani [amature pro boxing] wakaona ni vema wawape nafasi hiyo na kimsingi wamefuatilia na kurizika na maandalizi ya mabondia hao na wanaimani wataenda kufanya vema na kufuzu kuelekea nchini Brazil kutakofanyika fainali zenyewe za Olimpiki jijini Rio.

Aidha, Muta amesema mabondia hao watakaporudi wataungana na mabondia wengine wawili wa ridhaa Suleiman Kidunga na Swanga ambao watakwenda katika mashindano hayo kwa nafasi ya upendeleo kutokana na Tanzania kukosa mabondia waliofuzu moja kwa moja kupitia ushiriki wa michuano ya kufuzu.

Akimalizia Muta amesema pia kocha Mkenya ambaye ana sifa za nyota tatu kama ilivyoagizwa na kanuni za kamati ya kimataifa Olimpiki IOC za kuwaongoza mabondia katika mashindano hayo ataungana moja kwa moja na timu hiyo kwa maandalizi ya muda mfupi na baadaye kuelekea Rio Brazil kwa ajili ya fainali hizo zitakazopigwa mwezi Agosti.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali