Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mashine za Yanga zarejea dimbani

Ijumaa , 15th Dec , 2017

Wachezaji wa Yanga mshambuliaji Amisi Tambwe pamoja na kiungo Thabani Kamusoko ambao walikuwa majeruhi wa muda mrefu, wamerejea kikosini ambapo wanafanya mazoezi mepesi kwaajili ya kurejesha makali yao.

Afisa habari wa klabu hiyo Dismas Ten amesema klabu hiyo inaendelea na maandalizi ya michuano mbalinbali inayoikabili ikiwemo klabu bingwa ya Afrika ambayo wamepangwa kuanza na klabu ya St. Louis ya Shelisheli.

“Taarifa nzuri ni kwamba Kamusoko na Tambwe wameanza kufanya mazoezi, Tambwe anafanya mazoezi kwa asilimia mia moja na Kamusoko anaendelea na mazoezi mepesi ili kuweza kurejea kwenye ubora wake”, amesema Ten.

Ten ameongeza kuwa timu ina majeruhi mmoja, mlinzi wa kati Kelvin Yondani ambaye aliumia kwenye majukumu ya timu ya taifa ya Tanzania bara (Kilimanjaro Stars) iliyokuwa inashiriki michuano ya CECAFA na iliondolewa katika hatua ya makundi.

“Tuna majeruhi, Yondani ambaye aliumia akiwa na timu ya taifa na tayari daktari ameshathibitisha kuwa atakuwa nje hadi Desemba 28 ambapo ataanza mazoezi kwaajili ya kurejea uwanjani”, amemaliza Ten.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP