Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbao FC yajifariji kwa Wajelajela

Jumapili , 16th Apr , 2017

Timu ya Mbao FC ambayo ni miongoni mwa timu zilizo katika hatari ya kushuka daraja katika ligi kuu Tanzania Bara, baada ya kipigo cha 3-2 kutokwa kwa Simba, leo imepata faraja kama si matumaini baada ya kuibanjua Tanzania Prisons bao 1-0

Wachezaji wa Mbao FC katika moja ya mechi walizocheza Kaitaba Bukoba

Katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Nyamagana Jijini Mwanza, ukiwa ni mchezo wa kwanza wa ligi kuu kutumia uwanja huo tangu mwaka 1974, Mbao wamejipatia bao lao la pekee katika dakika ya 66 ya mchezo.

Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani wa wastani ukiwa umeanza kwa kupooza, Prisons walijikuta wakipata pigo katika kipindi cha kwanza baada ya mshambuliaji wake Jeremiah Juma kutolewa nje wa kadi nyekundu baada ya kubainika kumpiga kiwiko mchezaji wa Mbao FC, na kulazimika kucheza pungufu kwa karibu theluthi mbili ya muda wote wa mchezo.

Kwa matokeo hayo, sasa Mbao FC imefikisha point 30 na kupanda hadi nafasi ya 12 sawa na Ndanda FC huku Prisons ikibaki katika nafasi yake ya 9 na point 31.

Timu zilizo chini ya Mbao FC ni pamoja na Ndanda FC, Toto Africans, Majimaji na JKT Ruvu inayoshikilia mkia.

Katika mchezo mwingine, Mwadui FC imeishushia Ndanda FC kipigo cha mabao 4-2 katika mchezo uliopigwa Mwadui Complex Mjini Shinyanga, na kuifanya Mwadui ifikishe point 35 na kuchumpa hadi nafasi ya 6.

 

 

 

 

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi