Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbao wataja sababu ya kufungwa na Yanga

Jumatano , 23rd Mei , 2018

Kocha mkuu wa timu ya Mbao, Novatus Fulgence, amedai kuwa kukosekana kwa mshambuliaji wake tegemezi  Habib Kiyombo ambaye ni majeruhi ndiyo ilikuwa sababu kubwa iliyopelekea timu yake kupoteza mchezo dhidi ya Yanga.

Kocha huyo amesema hayo Mei 22, 2018 wakati akiongea na waandishi wa habari baaada ya kumalizika mchezo huo na kuongeza kuwa Habib Kiyombo ni mchezaji muhimu na ndiye mfungaji bora katika timu ya Mbao kwahiyo kukosekana kwake kumechangia timu hiyo kupoteza mchezo huo.

“Umuhimu wa Habib Kiyombo upo katika timu na ukizingatia yeye ndiye mfungaji bora katika timu yetu, kwahiyo kukosekana kwake kumepunguza kwa kiasi fulani asilimia za kushinda, lakini kingine ukiangalia katika mchezo wa kwanza yeye ndiye alitufungia magoli kwahiyo kutokuwepo kwake kumechangia sisi kupoteza nafasi za wazi ambazo tulizipata” amesema Fulgence 

Kocha Fulgence ameongeza kuwa alijaribu kutumia wachezaji wengi wa kikosi cha pili katika mchezo huo lengo likiwa ni kuwapa uzoefu kwaajili ya maandalizi ya msimu wa ujao wa ligi na kutaka kuonesha ubora wa wachezaji hao ingawa walikuwa hawapati nafasi mara kwa mara.

Jana Mei 22, 2018, katika mchezo wa Ligi Kuu Bara, timu ya Yanga ilishinda bao 1-0 katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam, goli pekee lilifungwa na kiungo Thabani Kamusoko kwa mpira wa adhabu katika dakika ya 26 na hivyo kuifanya klabu hiyo kufikisha alama 51 na kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali