Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mechi ya Simba na JKT Tanzania yaahirishwa

Jumatano , 3rd Apr , 2019

Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na JKT Tanzania uliokuwa upigwe katika dimba la Jamhuri mjini Morogoro, umeahirishwa kutokana na mvua.

Basi la Simba

Mvua kubwa iliyonyesha mchana mjini Morogoro, imesababisha Uwanja wa Jamhuri kujaa maji kiasi cha mpira kushindwa kudunda. Baada ya kusubiri kwa nusu saa, wasimamizi wa mechi wakaamua kuahirisha na kuahidi kuupangia ratiba nyingine.

Charles Mwakambaya ambaye ni Katibu wa chama cha soka mkoani Morogoro na msimamizi wa TFF kituo cha Morogoro, akizungumza baada ya mchezo kuahirishwa amesema kuwa hawatoweza kuipangia ratiba Simba kucheza kesho kwa sababu ya mchezo wa Klabu Bingwa Afrika, Jumamosi dhidi ya TP Mazembe.

"Hatuwezi kusema kuwa mchezo uchezwe kesho kwa sababu Simba ina ratiba ya mchezo wa TP Mazembe Jumamosi hii, kwahiyo wakicheza kesho tutakuwa tumwanyima masaa 48 ya kujiandaa dhidi ya mchezo mwingine", amesema Mwakambaya.

Kuhusu mashabiki ambao walishalipia tiketi zao, Mwakambaya amesema kuwa hela hazitorudishwa lakini utafanyika utaratibu mzuri na mambo yatakuwa sawa kwa mashabiki hao.

Simba sasa itarejea Jijini Dar es salaam kujiandaa na mchezo huo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe ambao inaelezwa kuwa wameshatua nchini.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa