Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mechi 3 za nusu fainali 'Sprite Bball Kings'

Jumanne , 4th Jul , 2017

Droo ya nne na ya mwisho ya kupanga ratiba ya michuano ya kikapu ya 'Sprite BBall Kings' imefanyika usiku wa kuamkia leo Jijini DSM kwa usimamizi wa Shirikisho la mpira wa kikapu Tanzania {TBF} kushirikiana na EATV LTD pia kushuhudiwa na timu shiriki

Mkuu wa vipindi vya East Africa Radio Nasser Kingu (Kushoto) na mtangazaji wa EATV, Suzy, wakiendesha droo ya nne kupanga ratiba ya michuano ya Sprite BBall Kings iliyofanyika usiku wa kuamkia leo.

Michuano hiyo itashirikisha timu nne (4) ambazo ni Kurasini Heat, TMT, Flying Dribblers pamoja na Mchenga BBall Stars pekee zilizoweza kufuzu hatua ya robo fainali kwa kuwafunga wapinzani wao mchezo uliyochezwa siku ya Jumamosi katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, mkuu wa vipindi vya East Africa Radio Nasser Kingu, amesema mechi hizo zitachezeshwa tofauti na ilivyokuwa katika mzunguko wa mtoano pamoja na robo fainali ulivyokuwa.

"Hongereni kwa kuingia hatua ya nusu fainali, mechi zinazofuata zitachezwa kwenye Julai 15, 22 na 29 mwaka huu, tumefanya hivyo ili tuweze kuwapa muda mzuri wa kufanya maandalizi yenu katika mapambano pia kuhusu suala la uwanja litatangazwa muda si mrefu, nawaomba mfuatilie na kuangalia EATV na kusikiliza East Africa Radio bila ya kusahau 'social network' zetu ili muweze kupata 'update' zote", alisema Nasser.

       Wawakilishi wa timu mbalimbali waliohudhuria kushuhudia droo ya wazi ya nne michuano ya Sprite BBall Kings.

Kwa upande mwingine, mshindi wa kwanza wa mashindano hayo anatarajiwa kuondoka na kitita cha shilingi milioni 10 akifuatiwa na mshindi wa pili kupata milioni tatu bila ya kumsahau mchezaji bora {MVP} kuondoka na shilingi milioni mbili.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya