Winga Machachari ,Benard Morrison akisaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Klabu ya Simba.
Nyota huyo ambaye alitikisa vilivyo tangu kufanyika kwa usajili wake , aliripotiwa kusaini mkataba wa miaka miwili katika klabu ya Yanga, lakini yeye alikanusha kuwa mkataba wake ungemalizika kati kati mwa mwezi Julai .
Uongozi wa Yanga , kupitia makamu mwenyekiti wa kamati ya mashindano Hersi Said alisema ''
“ Morrison alisaini mkataba wa miaka miwili mbele ya macho yangu ambao upo TFF na FIFA . Baada ya muda alikuja kuomba kuvunja mkataba huo kwa kuwa kapata timu yenye masilahi zaidi kwake .
Tuliligomea hilo kwa kuitaka hiyo klabu ije mezani kama klabu kusikiliza ofa yetu sio yeye . Hakuna mchezaji mkubwa kuliko klabu ya Yanga . Wanaomvuruga Morrison waje tu mezani wapewe ofa yetu tutamuuza bila shida “ Engineer Hersi Said.