Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwana Fa, Samatta, Flaviana Matata waipa dua Stars

Jumapili , 18th Nov , 2018

Watanzania pande zote duniani, leo wameungana katika kuiombea dua timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' katika mchezo wake wa kufuzu michuano ya mataifa ya Afrika dhidi ya Lesotho hii leo.

Kushoto ni Msanii wa Hiphop Mwana FA, katikati ni mwanamitindo Flaviana Matata na kulia ni Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta.

Stars inazisaka alama tatu muhimu ili kujihakikishia nafasi ya kufuzu kwa asilimia 100 michuano hiyo itakayofanyika mwakani nchini Cameroon kwa jumla ya alama nane, huku isubiri kumaliza mchezo wa mwisho dhidi ya Uganda ambao hautokuwa na madhara yoyote endapo itashinda mchezo wa leo.

Mastaa mbalimbali kutoka pande zote wameonesha uzalendo mkubwa na kuguswa na mchezo huo, wakiiombea Stars kuibuka na ushindi utakaoweka historia ya kushiriki mara ya pili kwa Tanzania kwenye michuano hiyo.

Mbwana Samatta ambaye ni nahodha wa Taifa Stars atakosekana katika mchezo huo kutokana na kuoneshwa kadi mbili za njano kwenye michezo miwili mfululizo. Katika kuiombea timu yake ameandika,

"Mungu baba tunakuomba utupe sisi ata goli moja wao uwanyime, ila ata ukitupa mawili nayo sio mbaya baba, ata uwe mduki wa Msuva ata kichwa cha Bocco sisi baba fresh kabisa au baba fanya ata miujiza Ulimwengu afunge na kushoto baba ata Aishi akiubutua uingie moja kwa moja baba yetu ameen ", ameandika katika ukurasa wake wa Twitter.

Msanii nguli wa muziki wa HipHop nchini, Mwana Fa naye ameitakia kila la heri Taifa Stars katika mchezo huo kwa kuandika, "Ona pamoja na kelele zote hizi za mpira sijawahi kuiona nchi yangu ikicheza fainali za kombe la Africa TOKA KUZALIWA. Tupo karibu sana na Cameroon 2019 safari hii, karibu mno..Kwa uwezo wa Mungu, tuvuke kamlango haka..bahati njema brothers, tupelekeni Cameroon."

Mwanamitindo wa Tanzania anayeishi nchini Marekani, Flaviana Matata ameonesha uzalendo kwa taifa lake kwa kuandika, "Good luck to Taifa Stars, AFCON2019", katika ukurasa wake wa Twitter.

Taifa Stars imeshiriki mara moja pekee katika michuano ya mataifa ya Afrika, ambayo ni mwaka 1980 nchini Nigeria. Nafasi ya mwaka huu ni nafasi pekee ambayo itaweka historia kwa mara ya pili kushiriki michuano hiyo baada ya takribani miaka 38.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali