Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwenyekiti Yanga akiri maji kuzidi unga

Jumanne , 10th Dec , 2019

Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Dkt. Mshindo Msolla ametoa ufafanuzi juu ya mapato na matumizi ya klabu hiyo tangu uongozi wake ulipoingia madarakani, Juni 2019, huku akibainisha uwepo wa madeni ambayo wamerithi kutoka kwa uongozi uliopita.

Mwenyekiti wa Yanga Mshingo Msolla (suti ya kijivu waliokaa) akiwa na mashabiki wa Yanga.

Msolla amesema gharama za kuendesha timu ni kubwa, kuliko mapato yanayoingia, huku wakiwa wamerithi madeni makubwa kutoka katika uongozi uliopita ambayo inabidi yalipwe au kupunguzwa kadri inavyowezekana.

"Nimeamua kuja kwenu Waandishi ili nitoe ufafanuzi juu ya mapato na matumizi ya klabu yetu. Tulivyoingia madarakani tulikuta timu madeni makubwa ambayo tumejitahidi kuyapunguza huku bado tukitakiwa kuiendesha timu", alisema Msolla.

Mwenyekiti huyo ametaja madeni makubwa ya aina nne waliyorithi kama ifuatavyo:-

1. Serikali (Mamlaka ya Mapato Tanzania 'TRA' shilingi milioni 800), 

2.Ada ya uhamisho ya wachezaji waliosajiliwa miaka miwili iliyopita shilingi milioni 254.

3. Madeni ya makocha na wachezaji waliopita (Hans Van Pluijm, George Lwandamina, Youthe Rostand, Donald Ngoma na Obrey Chirwa) jumla shilingi milioni 600.

4. Watu binafsi shilingi milioni 237

5. Gharama za Usajili wa timu za wakubwa na ile ya Wanawake shilingi milioni 600.

Msola ametaja vyanzo vya mapato vya klabu hiyo ambayo ni SportPesa, KCB, Vodacom, Azam TV, GSM, Yanga TV na kampuni ya Maji ya Afya, ambayo kwa mwaka wanapata shilingi bilioni mbili wakati gharama za kuiendesha timu ni Bilioni nne.

Aidha Msolla amewaahidi wanachama wa timu hiyo kuwa, mpaka Mei 2020, watakuwa wameingia katika mfumo wa uwekezaji kwa njia ya hisa. Amesema watawashirikisha Wanachama katika kila hatua ili maamuzi yawe ya watu wote.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali