Jumatatu , 4th Feb , 2019

Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai amethibitisha kupokea barua ya mbunge wa Mtama Mh. Nape Nnauye kujiuzulu nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

Nape Nnauye

Kagaigai amesema leo Jumatatu Februari 04, 2019 Nape ameandika barua kwenda kwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ya kujiuzulu nafasi hiyo na tayari spika amempatia nakala ya barua hiyo.

''Ni kweli nimeiona barua aliyomwamndikia Spika na mimi nimepata nakala yangu kwahiyo ni kweli amejiuzulu labda awe na mawazo mengine'', amesema.

Hata hivyo www.eatv.tv imemtafuta Nape Nnauye ambaye alipokea simu yake kisha kusema yupo kwenye kikao hawezi kuendelea na maongezi. ''Nipo kwenye mkutano siwezi kuongea'', alisema.

Machi mwaka 2017, Nape aling’olewa kwenye nafasi ya Uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo sasa ipo chini ya Waziri Harrison Mwakyembe.