Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nasreddine Nabi awatuliza wanayanga, tupo tayari

Ijumaa , 24th Sep , 2021

Kocha mkuu wa Yanga SC, Mohamed Nabi amesema kuwa wamejiandaa vyema kuelekea mchezo wa Jumamosi ya kesho Septemba 25, 2021 wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba SC huku akiweka wazi kuwa atatoa nafasi kwa wachezaji wanaostahili kuanza mchezo huo.

Kocha wa klabu Yanga, Mohammed Nasreddine Nabi akiongea mbele ya Wanahabari.

Nabi amesema kauli hiyo leo Septemba 24, 2021 mbele ya waandishi wa Habari kuwa kikosi kipo na hali nzuri kuelekea mchezo mkubwa unaofuatiliwa ndani na nje ya Tanzania, huku akionesha hali kusikitishwa na kanuni ya kutumia wachezaji nane tu kwenye michezo iliyopo chini ya TFF, huku akisema hana budi kuheshimu sheria iyo.

Mtunisia huyo amewaomba wanayanga wawe na uvumilivu kuelekea msimu mpya kwakuwa wanakikosi kizuri kuelekea msimu mpya na pindi pale timu itakapokuwa namuunganiko mzuri itakuwa tishio sana.

Pia amewashukuru viongozi wa Yanga kwa kufanya usajili wa viwango vikubwa pamoja na kuwa wavumilivu pindi matokeo yaponakuwa sio ya kuridhisha hii ikiwemo pamoja na kutolewa kwenye mashindano ya ligi ya mabingwa kwenye hatua za awali msimu huu. 

Kwenye hali za majeruhi, Nabi ametabanaisha kuwa wachezaji kama Balama Mapinduzi aliyekosa msimu uliopita na Yassin Mustafa aliyekaa nje kwa miezi sita kabla ya msimu kutamatika, watahitaji kupitia maandalizi na mazoezi mepesi kabla ya kurejesha katika hali ya ushindani.

Vile vile Yanga, watamkosa Mukoko Tonombe, ambaye alipewa kadi nyekundu katika fainali hiyo baada ya kupiga kiwiko kwa makusudi nahodha wa Simba, John Bocco na kupelekea mwamuzi wa mchezo huo Ahmed Arajiga kumtoa nje.

Kuelekea michezo huu wa kukata na shoka pande zote mbili zimefanya usajili yakinifu kuelekea msimu mpya, hivyo nafasi za wachezaji hawa wawili kwa timu zote mbili hazitakuwa na kazi ya kuziziba pindi watakapo shuka kugombea taji la kwanza la msimu huu.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ