
Mshambuliaji Mrisho Ngassa.
Kutoka nchini Afrika Kusini, Ngassa amesema kwamba ameanza mazoezi kuhakikisha anajiweka fiti na ni mazoezi ya taratibu sana.
Ngassa amekaa takribani mwezi nje ya uwanja akiuguza maumivu ya goti na baadaye alifanyiwa upasuaji huo ambao ulikwenda vizuri kwa mujibu wa madaktari.
Kiungo huyo raia wa Tanzania mwenye kasi, amesema ana imani kubwa mambo yataenda vizuri baada ya muda si mrefu na kurejea tena dimbani.