Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ngorongoro Heroes kusuka au kunyoa leo, AFCON U20

Jumatatu , 22nd Feb , 2021

Timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 20 'Ngorongoro Heroes', saa 4:00 usiku wa leo Februari 22,  2021 inataraji kushuka dimbani kucheza dhidi ya Morocco U20 kwenye mchezo wa mwisho kundi C kuwania nafasi ya kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya AFCON U20 nchini Mauriatania.

Wachezaji wa Ngorongoro Heroes wakifanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuwavaa Morocco leo.

Kuelekea kwenye mchezo huo ambao Ngorongoro Heroes wanahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini ya kutinga hatua hiyo, Nahodha wa timu hiyo Kelvin John amesema wanaamini watafuzu kutokana na walivyojipanga  kwenda  kupata matokeo mazuri.

“Tunajua Morocco ni timu nzuri na sisi tumejipanga kwenda kupata matokeo kwenye mchezo huo, bado tuna nafasi kubwa ya kuweza kupata matokeo kwahiyo, kikubwa zaidi tunapokea maelekezo vizuri kutoka kwa mwalimu wetu na mipango yake ili tuweze kufanya vizuri kwenye mchezo  huo”.

Kwa upande wa kocha wa kikosi hicho, Jamhuri Kihwelo 'Julio', amesema “Tunakutana na Morocco, hatuogopi ushindani huu uliopo kwa wenzetu waliotangulia kabla yetu, lakini tunasema tu, kubwa tunataka tushinde ili tupate nafasi ya kuendelea”.

Ngorongoro Heroes ikipata ushindi, itafikisha jumla ya alama 4 na kuombea mchezo wa Gambia dhidi ya Ghana utakaochezwa muda mmoja umalizike kwa sare ili wamalize nafasi ya tatu na kufuzu kwakuwa 'Best loser' kwani Tunisia kutoka kundi B imefuzu ikiwa best loser kwa kuwa na alama 4.

Kundi A, wenyeji Mauritania wameshika nafasi ya tatu wakiwa na alama 3 hivyo wataweza kufuzu hatua ya robo fainali endapo Ngorongoro Heroes na Gambia kutoka kundi C watafungwa ama kutoka sare na wawili hao kusalia na alama  mbili mbili.

Timu tano zilizofuzu kucheza hatua ya robo fainali ni, vinara wa kundi A, Cameroon, Uganda walioamliza wapili, Kundi B, Burkina Faso, Central Afrika na Tunisia ikiwa ni 'Best loser'.

Hatua ya robo fainali ya michuano hii ambayo Ngorongoro Heroes wanashiriki kwa mara ya kwanza, inatazamiwa kuchezwa siku ya Alhamisi ya tarehe 25 Februari 2021 nchini Mauritania ambao ndiye wenyeji wa michuano hiyo.

HABARI ZAIDI

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani