Ijumaa , 22nd Oct , 2021

Wakati wachezaji John Bocco, Aishi Manula, Mohammed Hussein na Fei Toto kuondoka na tuzo za TFF usiku wa jana, Benard Morrison anasema aliambulia kurudi na chupa ya maji nyumbani.

Picha ya mchezaji Benard Morrison

Kupitia ukurasa wake wa Instagram mchezaji huyo asiyeishiwa na vituko ameandika kuwa tuzo pekee aliyoshinda ni nguo bora ya ndani ya msimu.

"Kwa hivyo jana usiku wengine walipokwenda nyumbani na tuzo, mimi nilikwenda nyumbani na chupa ya maji, lazima nikuambie kabla ya kuanza kusema nimeshinda nguo bora ya ndani ya msimu, kila mtu alistahili hongera kwa wote".