Jumamosi , 23rd Jan , 2021

Timu ya taifa ya Tanzania ‘taifa stars’ itaendelea kuwakosa nyota wake John Bocco,Ibrahim Amen na Erasto nyoni walioripotiwa kuwa majeruhi, wakati ikitarajiwa kutupa karata yake ya pili kwenye michuano ya CHAN mchezo wa kundi D leo usiku dhidi ya timu ya taifa ya Namibia, utakaochezwa Saa

Taifa stars itaendelea kuikosa huduma ya wachezaji wake wakongwe na wazoefu John Bocco na Erasto Nyoni kwenye mchezo dhidi ya Namibia kutokana na majeruhi

Taifa stars ilipoteza mchezo wa kwanza kwa kufungwa mabao 2-0 na timu ya taifa ya Zambia, na sasa kikosi hicho kinachonolewa na kocha Mrundi Etienne Ndayiragije kinahitaji matokeo ya ushindli kwenye mchezo wa usiku wa leo ili kufufua matumaini ya kusonga mbele kwenye fainali hizo za CHAN.

Namibia wao ndio wanaburuza mkia kwenye kundi hilo baada ya kufungwa mabao 3-0 na timu ya taifa ya Guinea kwenye mchezo wa kwanza, hivyo Taifa stars wapo juu ya Namibia kwenye msimao wa kundi wakiwa nafasi ya 3 kutokana na tofauti ya mabao ya kufungwa, Guinea ndio vinara wa Kundi D wakiwa na alama 3 sawa na Zambia, Guinea wakikaa kileleni kwa faida ya mabao ya kufunga.

Mara ya mwisho Timu hizi kukutana ilikuwa Machi 5, 2014. mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.