Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rasmi Yanga yapokea rasimu kutoka La Liga

Jumatano , 2nd Dec , 2020

Mwenyekiti wa Kamati ya Mabadiliko ya Yanga SC, Wakili Alex Mgongolwa, leo Desemba 2, 2020 amekabidhi rasmi kwa uongozi rasimu ya awali ya mfumo wa mabadiliko.

Akiongea kabla ya kukabidhi rasmi hiyo ambayo imeandaliwa kwa ushirikiano wa kamati hiyo na kamati ya La Liga pamoja na washauri mbalimbali wa ndani na nje ya Nchi, Mgongolwa amesema sasa rasmi klabu inarudi kwa wananchi.

''Tuna vipaumbele viwili kwenye rasmi yetu ya mfumo wa mabadiliko, kutakuwa na Menejimenti imara ili kuwa na taasisi bora lakini pia Wanachama wetu hatujawaacha nyuma, wao kitaalam wametambulika kama 'Fans Engagement' ambao wanatambulika rasmi na mfumo'' - Alex Mgongolwa.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Mabadiliko ya Yanga Mhandisi Hersi Said amesema, ''Leo Yanga SC tunaandika historia kwa kuleta mfumo wa uendeshaji wa klabu yetu kutoka kwenye Dunia ya kwanza kwenye soka kwa maana ya La Liga Hispania''.

Hersi ameongeza kuwa, ''Mfumo huu unakwenda kuirudisha klabu kwa wanachama na wao ndio watakuwa wamiliki halali wa klabu na baada ya mfumo kukamilika, niwahakikishie tu watu wote sio tu Tanzania bali Afrika nzima watakuja kwetu kujifunza''.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Yanga Dkt. Mshindo Msolla, amepokea rasimu hiyo na kuikabidhi kwa Mshauri wa Mabadiliko wa klabu hiyo Senzo Mbatha ili aipitie na mchakato uendelee.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP