Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rekodi kubwa 5, ubingwa wa 19 wa Liverpool

Ijumaa , 26th Jun , 2020

Klabu ya soka ya Liverpool imefanikiwa kushinda ubingwa wa ligi nchini Uingereza kwa mara ya kwanza baada ya miaka 30 na kufikisha ubingwa wa 19 nyuma ya mahasimu wao Man United wenye mataji 20.

Liverpool FC

Ni baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Chelsea na Manchester City, ambao ndiyo walikuwa kizuizi kwa Liverpool katika kushinda ubingwa kutokana na kuwepo kwa uwezekano wa kuzifikia pointi zake kabla ya mchezo huo wa jana.

Mabao 2-1 waliyoshinda Chelsea kupitia kwa Willian na Christian Pulisic yalitosha kupelekea furaha Anfield na kuzalisha rekodi mbalimbali.

Rekodi ya pili: Liverpool imeshinda ubingwa zikiwa zimebakia mechi 7 ligi kuisha, ikiwa ni klabu ya kwanza kufanya hivyo ikiizidi rekodi iliyowekwa na klabu za Man United (1907/08 na 2000/01), Everton (1984/85) na Man City (2017/18).

Rekodi ya tatu: Msimu wa 2019/20 umekuwa msimu wa tatu kati ya sita ya hivi karibuni ambayo mechi ya kuamua ubingwa imechezwa katika uwanja wa Stamford Bridge, mechi zingine ni Chelsea Vs Crystal Palace 2014/15 na Chelsea Vs Tottenham 2015/16.

Rekodi ya nne: Ubingwa wa Liverpool umekuwa na mkusanyiko wa rekodi kadhaa ambazo wamezipata ndani ya msimu huu, ikiwemo kushinda mechi 18 mfululizo, kushinda mechi 23 mfululizo za nyumbani, kushinda ubingwa wa ligi kwenye miongo 8 tofauti na kutokufungwa katika mechi 44 za mashindano yote.

Rekodi ya tano: Msimu huu Liverpool imeifunga kila klabu iliyokutana nayo katika ligi angalau mara moja, ikiwa ni historia ambayo haijawahi kuwekwa na klabu hiyo hapo kabla.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali