Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rekodi za Joshua na Povetkin kuelekea pambano lao

Jumatatu , 16th Jul , 2018

Pambano la uzito wa juu la kuwania mikanda ya ubingwa wa dunia kati ya mabondia Anthony Joshua anayelinda mikanda yake ya IBF, WBA (Super), WBO na IBO dhidi ya Alexander Povetkin anayeshikilia mkanda wa WBA (Regular) limetangazwa kufanyika Septemba 22, 2018.

Bondia Anthony Joshua

Pambano hilo ambalo litapigwa kwenye uwanja wa Wembley jijini London nchini Uingereza, linatarajiwa kuwa na ushindani kutokana na mabondia hao kubobea kwenye upande wa 'KO'. Joshua ana rekodi ya kushinda kwa KO mapambano 20 kati ya 21 huku Povetkin ameshinda mara 24 kwa KO kati ya 34.

Joshua mwenye umri wa miaka 28 ana rekodi ya kutopoteza pambano hata moja tangu aanze kupigana akiwa ameshinda mapambano yote 21 aliyopanda ulingoni huku mpinzani wake Povetkin mwenye miaka 34 akiwa na rekodi ya kupoteza pambano 1 kati ya 35 aliyopigana.

Joshua atakuwa anarejea kwenye uwanja wa Wembley kwa mara ya kwanza tangu alipopigana pambano la mwisho  dhidi ya Wladimir Klitschko April 2017 ambapo mashabiki 90,000 walihudhuria pambano hilo lililomalizika kwa Joshua kushinda kwa 'TKO'.

Bondia Alexander Povetkin

Kabla ya pambano la Septemba 22, Joshua amepigana mara mbili dhidi ya Carlos Takam na Joseph Parker mapema mwaka huu na alishinda yote kwa KO. Kwa upande wake Povetkin pambano la mwisho alishinda kwa KO dhidi ya David Price wa Uingereza. 

Mshindi wa pambano hilo atabeba mikanda mitano ya uzito wa juu yaani minne ya IBF, WBA (Super), WBO  na IBO aliyonayo Joshua na ule mmoja wa WBA (Regular) alionao Povetkin.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa