Jumanne , 20th Dec , 2022

Taarifa kutoka nchini Hispania zinaripoti kuwa mchezaji bora wa dunia mara tano (5) Cristiano Ronaldo anatarajia kusaini mkataba wa miaka 2 na nusu  na klabu ya  Al Nassr ya Saudia Arabia mwishoni mwa mwaka huu, mkataba utakaomalizika Juni 2025.

Mshambuliaji Cristiano Ronaldo

 Thamani ya mkataba huo inatajwa kuwa ni Euro millioni 200 kwa msimu, hivyo mpaka utakapomalizika inatarajiwa kufikia Euro milioni 500 ambayo ni zaidi ya Trion 1, bilioni 238 na milioni 178 kwa pesa ya Tanzania.

Ronaldo raia wa Ureno  mwenye umri wa miaka 37, kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kuvunja mkataba na klabu ya Manchester United kwa makubaliano ya pande zote mbili. Kwa upande mwingine imekuwa ikiripotiwa kuwa Ronaldo bado anataka kuendelea kucheza soka barani Ulaya na anamatamanio yakucheza kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.