Farid Musa
Afisa habari wa klabu hiyo Jaffary Iddy Maganga amesema kilichokuwa kikisubiriwa ni vibali vya Farid kufanya kazi nchini Hispania na siyo kweli kwamba klabu hiyo ilikuwa ikimbaia.
"Waliokuwa wanasema tunamzuia Farid kwenda Hispania, kwanini hawajiulizi ni kwanini tulimruhusu aende kufanya majaribio, mchakato ulikuwa unaendela ikiwemo kupata vibali vya kazi, sasa kila kitu kiko tayari na ataondoka muda wowote kwenda kujiunga na klabu yake mpya ya Tenerife" amesema Maganga
Kwa upande wake Farid Mussa amethibitisha, kila kitu alichokuwa anasubiria kimeshakamilika na anachosubiria kwa sasa ni muda wa kuondoka kuelekea nchini Hispania katika timu ya Tenerife.