Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Samatta aelezea ndoto yake, Klabu Bingwa Ulaya

Jumanne , 10th Sep , 2019

Nahodha wa Taifa Stars na mshambuliaji wa klabu ya Genk, Mbwana Samatta amezungumzia masuala mengi yanayoihusu Taifa Stars pamoja na klabu yake ya Genk.

Mbwana Samatta

Mahojiano hayo yamefanyika alipokuwa kambini na Taifa Stars katika michezo miwili ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia, ambapo pamoja na mambo mengine mengi, Samatta ameonesha kufurahishwa na mbinu za kocha Etienne Ndayiragije, akisema  kuwa zinawasaidia kuwa na ari ya kupambana uwanjani na kuahidi kufanya makubwa chini yake.

Samatta amesema kuwa ndoto kubwa anayoiota kwa sasa ni siku moja kuja kucheza michuano ya Kombe la Dunia, japo hana matumaini ya nchi yake kufikia hatua hiyo kutokana na ugumu uliopo.

Kuhusu kuwepo katika kikosi cha Genk kitakachoshiriki michuano ya Klabu Bingwa Ulaya msimu huu, ikipangwa na timu vigogo kama Liverpool na Napoli, Samatta amesema kuwa kwake ni jambo kubwa sana kupata nafasi ya kucheza katika uwanja wa klabu ya Liverpool (Anfield) kwakuwa ni klabu kubwa, huku akieleza kuwa binafsi alipendelea angepangwa kundi moja na Barcelona au Real Madrid za Hispania.

"Unaposhiriki michuano ya Klabu Bingwa Ulaya huwezi kukosa kukutana na vigogo kama hao, mabingwa wa nchi mbalimbali. Lakini mimi ningependa zaidi ningekutana na Barcelona au Real Madrid, ila hata hivyo Anfield pia ni moja ya sehemu bora sana, si mbaya kucheza na timu kama Liverpool na Napoli ", amesema.

Ikumbukwe kuwa Samatta anakuwa Mtanzania wa kwanza kucheza michuano ya Klabu Bingwa Ulaya, ambapo katika kundi la Genk kuna timu za Liverpool, Napoli na RB Salzburg. Pia atacheza kwa mara ya kwanza katika ardhi ya Uingereza pindi atakapovaaana na Liverpool katika dimba la Anfield.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi