Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba na Yanga hakuna mafanikio - Uhuru Seleman

Jumatatu , 20th Feb , 2017

Mchezaji wa Kimataifa wa Tanzania anayechezea timu ya Royal Eagles ya nchini Afrika kusini Uhuru Seleman amefunguka na kusema mafanikio yake yamekuja baada ya yeye kutoka katika vilabu vya Tanzania na kwenda nje. 

Uhuru Seleman

 

Uhuru amesema licha ya kuchelewa kutoka katika soka la nyumbani lakini angalau yeye amepata mafanikio ambayo anajivunia kwa sasa, kama vile kuweza kumiliki nyumba zake mwenyewe binafsi, kumiliki biashara mbalimbali na kuweza kuhudumia familia yake. 

"Naweza sema mimi nimechelewa sana kutoka katika soka la nyumbani, lakini hata hivyo bado najivunia vitu kadhaa ikiwemo kuwa na makazi binafsi zaidi ya nyumba moja,  kumiliki biashara na kuhudumia familia bila kuteteleka kwa lolote lakini nikukumbushe tu kuwa kucheza Simba na Yanga siyo wote wanaopata mafanikio unayoyafikiria, mimi vitu vingi nimetimiza baada ya kutoka nje" alisema Uhuru Seleman

Mbali na hilo Uhuru Seleman amezungumzia mchezo ambao utafanyika siku ya tarehe 25 kati ya watani wa jadi Simba na Yanga.

"Kiukweli sijaziangalia timu zilivyo kwa muda mrefu sasa lakini huwa mechi ya Simba na Yanga ni ngumu kuitabiri ukiwa nje ya uwanja" alisema Uhuru Seleman 

Uhuru Seleman anasema kwa sasa yeye hachezi mpira kama mapenzi bali anacheza mpira kama kazi hivyo anaangalia maslahi na kama Simba watamuhitaji tena kuja kucheza katika klabu hiyo hana tatizo ataangalia tu maslahi yake na si kitu kingine.

"Mpira kwangu ni kazi na sichezi mpira kwa mapenzi, ikitokea Simba wananihitaji nitakwenda kukiwa na maslahi katika hilo" alisisitiza Uhuru Seleman 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi