Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yapotea njia kwenye mashamba ya miwa

Jumatano , 18th Jan , 2017

Vinara wa ligi kuu Tanzania Bara imeanza kupoteza mwelekeo wa njia ya ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara baada ya leo kupotea njia kwenye mashamba ya miwa, na kulazimishwa suluhu na wakata miwa wa Mtibwa Sugar

Kiungo wa Mtibwa Ally Shomari akipambana na beki wa Simba Hamad Juma

Katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Jamhuri mjini Morogoro, Simba imeendelea kuonesha 'ubutu' katika safu yake ya ufungaji kwa kutengeneza nafasi nyingi lakini ikishindwa kuzitumia.

Kwa upande wa Mtibwa, waliingia uwanjani wakionesha kukamia mchezo huku wakiwa na mbinu ya kumaliza kwa sare kwa kuweka ukuta imara ulioongozwa na wakongwe Henry Joseph Shindika, Salim Mbonde, Vincent Barnabas, Issa Rashid 'Baba Ubaya' na kiungo Shaaban Nditi, hali iliyopelekea mchezo huo umalizike bila bao kwa upande wowote.

Akizungumzia mchezo huo, Nahodha wa Simba Jonas Mkude amekubali matokeo na kusema mpira una matokeo matatu, hivyo licha ya kutoyapenda, inabidi wayakubali kwa kuwa ndiyo matokeo ya mpira, na kuahidi kufanya vizuri zaidi katika michezo inayofuata.

Mshambuliaji wa Simba Shiza Kichuya baada ya kumfanyia madhambi Rashidi Mandawa  katika mchezo wao wa ligi kuu, Morogoro

Kwa upande wake Nahodha wa Mtibwa Sugar Shaaban Nditi ameshukuru kupata point moja katika mchezo huo, huku akitupia lawama ubovu wa uwanja na kusema wao hawakuzoea kufanya mazoezi katika uwanja huo, hivyo ubovu wa uwanja umechangia kuikosesha timu yake ushindi katika mchezo wa leo.

Matokeo haya yanaifanya Simba iendelee kubaki kileleni kwa kufikisha point 45, ikiwa ni point 2 mbele ya Yanga

Simba na Mtibwa ni timu ambazo wachezaji wake wengi wamewahi kuzichezea timu zote mbili yaani kuna wachezaji wa Simba waliotoka Mtibwa na kuna wachezaji wa Mtibwa waliotoka Simba, hivyo ni timu ambazo wachezaji wake wengi wanafahamiana

Mchezi ya Simba Vs Mtibwa katika mzunguko wa Kwanza ambapo Simba walishinda 2-0 katika uwanja wa Uhuru

 

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini