Jumanne , 18th Oct , 2016

Mchezaji wa zamani wa timu za Taifa za Raga za Kenya, kwa wachezaji 7 na 15, Innocent Simiyu ameteuliwa kuwa Kocha wa Timu ya Taifa hilo ya wachezaji 7.

Innocent Simiyu

Simiyu, alikuwa nahodha wa timu ya Kenya Sevens, kati ya 2006 na 2008, na nahodha wa timu ya Kenya 15 katika kipindi cha 2008 hadi 2011.

Amekabidhiwa timu hiyo inayojiandaa na mashindano ya Rugby 7, ambapo Desemba 2-3 itacheza kwenye Mashindano ya Dunia ya Dubai 7.

Kenya wapo kwenye kundi D, na timu za Ufaransa, Japan na Australia, kutafuta nafasi ya fainali itakayofanyika London, Mei 20-21 mwakani.