Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Solskjaer amehoji maamuzi ya vilabu vya EPL

Ijumaa , 30th Oct , 2020

Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer amehoji ni kwanini vilabu vya Ligi Kuu England vilipiga kura ya kupinga kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwenye michezo ya EPL msimu huu.

Mchezo dhidi ya Arsenal siku ya Jumapili utakuwa wa 100 kwa kocha Ole Gunnar Solskjaer akiisimamia Man United kama kocha mkuu

Kura ya vilabu kupinga kanuni ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwa mchezo mmoja ilipigwa mwezi Agosti na vilabu vinavyoshiriki ligi kuu England EPL na kutumia kanuni ya zamani ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 3.

Lakini kanuni hiyo bado inatumika kwenye michuano ya klabu bingwa ulaya na ile ya Europa league.

“Sielewi na siamini kwanini ilipigwa kura ya kupinga, tunapaswa kuwalinda na kuwafikiria wachezaji ” alisema Solskjaer alipokuwa akiongeza na waandishi wa habari kuelekea mchezo dhidi ya Arsenal.

Kutokana na mlipuko wa Covid-19 ambao ulisababisha ligi mbali mbali kusimama Duniani kote na wachezaji kushinda kufanya mazoezi, ili kulinda afya za wachezaji kuwaepusha na majeruhi, vilabu vilipewa nafasi ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwa mchezo kutoka wa 3.

Shirikisho la soka Dunia FIFA lilitoa ruhusa kwa ligi mbali mbali kendelea kutumia kunani hiyo kwa muda mpaka mwishoni mwa msimu huu wa 2020-21, lakini vilabu vya England vilipiga kura ya kupinga kununi hiyo na kutumia kanuni ya zamani ya mabadiliko ya wachezaji wa 3.

Ole Gunnar sio kocha wa kwanza kuhoji juu ya umuhimu wa mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwani hata Kocha wa Manchester City Pep Guardila anaamini afya za wachezaji zinapaswa kulindwa huku Kocha wa Chelsea, Frank Lampard akisisitiza makosa yalifanyika kupinga kanuni ya mabadiliko .

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa