Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Steve Bruce kuvunja uteja kwa Arsenal leo?

Jumatatu , 18th Jan , 2021

Ligi kuu nchini England inatazamiwa kuendelea usiku wa leo tarehe 18 Januari 2021 kwa mchezo mmoja, 'Washika mitutu wa jiji la London' klabu ya Arsenal itawakaribisha Newcastle United inayonolewa na kocha Steve Bruce mchezo utakaochezwa sa 4:00 usiku leo kwenye dimba la Emirates.

Kocha wa klabu ya Newcastle United, Steve Bruce.

Kuelekea kwenye mchezo huo, Arsenal itamkosa mlinzi wake wa kati Pablo Mari ambaye anasumbuliwa na maumivu ya misuli ya nyuma ya goti aliyoyapata kwenye mchezo uliopita dhidi ya Crystal Palace na kumfanya afanyiwe mabadiliko baada ya maumivu kumzidia.

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta amesema kuna hati hati kama mlinzi wake wa kushoto Kieran Tierney anayesumbuliwa na maumivu ya misuli na mshambuliaji wake Gabriel Martinelli mwenye maumivu kwenye kifundo chake cha mguu kama wataweza kucheza kwenye mchezo huo.

Taarifa nzuri kwa washika mitutu hao wa jiji la London ni kwamba, kiungo wake mpya Thomas Partey aliyesajiliwa dirisha kubwa la usajili lililopita anatazamiwa kurejea dimbani baada ya kupona maumivu  kwenye kifundo chake cha mguu na mlinzi Gabriel Magalhaes kuripitiwa kuwa fiti kuwavaa Newcastle

Kwa upande Newcastle United inayonolewa na kocha Steve Bruce, itamkosa winga wake Ryan Fraser anayetumikia aadhabu ya kukosa mchezo mmoja baada ya kuoneshwa kadi mbili za njano kwenye mchezo uliopita na kiungo Jonjo Shevley atakosekana baada ya kufanyiwa upasuaji wa paja.

Walinzi wa kati na nahodha wa Newcastle Jamal Lascelles na nahodha msaidizi Federico Fernandez hawana uhakika wa kuwemo kikosini baada ya kukutwa na Covid-19 hivyo watasubiri majibu ya vipimo vya mwisho kuonesha kama wapo fiti ama laa.

(Kwenye picha: Ni kiungo mshambuliaji wa Arsenal, Eddie Smith Rowe akipiga mpira na kuifungia Arsenal bao la pili kwenye ushindi wa Arsenal wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle kwenye kombe la FA siku tisa zilizopita.)

Mchezo huo ni fumbo kwa kocha wa Newcastle United Steve Bruce kutokana na rekodi yake mbaya mbele ya Arsenal kwenye dimba la Emirates ambapo amecheza michezo 11 dhidi ya Arsenal na kufungwa michezo 8 na kuambuliwa sare tatu bili ushindi akiwa ugenini dhidi ya Arsenal.

Leo wafuatiliaji wa soka Ulimwenguni watasubiri kuona kama kocha huyo atavunja uteja akiwa ugenini mbele ya Arsenal baada ya mchezo kumalizika. Kwa upande wa Arsenal na wenyewe hawana rekodi nzuri kwenye dimba lao hilo msimuu, wamecheza michezo 8 lakini wameshinda mchezo 1 tu.

Kwa rekodi hiyo, maana yake Arsenal wameambulia alama 5 kati ya 21 zilizotarajiwa kama wangepata ushindi kwenye michezo 7 waliyocheza na badala yake kushinda mchezo 1 pekee, kutoa sare 2 na kufungwa michezo 4 kwenye dimba la Emirates kwenye EPL msimu huu.

Arsenal ambaye wameifunga Newcastle mabao 2-0 siku 9 zilizopita na kuwatoa kwenye mzunguko wa tatu wa kombe la FA, huenda wakiingia kifua mbele na rekodi yao nzuri mbele ya Newcastle ya kuwafunga mara 14 kwenye michezo 15 ya mwisho waliyocheza tokea wafungwe 2010 bao 1-0.
 

HABARI ZAIDI

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi