Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Taifa Stars kuanza na Zambia leo michuano ya CHAN

Jumanne , 19th Jan , 2021

Timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' inatazamiwa kutupa karata yake ya kwanza kwenye michuano ya CHAN inayofanyika nchini Cameroon kwa kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya timu ya taifa ya Zambia 'Chipopolo' saa 1:00 usiku kwenye dimba la Omniport jiji la Limbe.

Kikosi cha Taifa Stars kikifanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuwavaa Zambia.

Kuelekea kwenye mchezo huo, kocha wa Taifa Stars, Mrundi Etienne Ndayiragije amesema “maandalizi yameenda vizuri, wachezaji wapo sawa. Kuhusu korona wamechekiwa wote wako sawa, tuko vizuri. Tunaendeelea kujiandaa kwenye vile ambavyo tunaamini vitakuwa vya msaada kwetu”.

Kuhusu nafasi ya Stars kwenye mchezo huo, Ndayiragije amesema “ morali na hali ya kujiamini kuko juu kwenye kambi, wachezaji wapo tayari kwa mchezo, nimewaambia tutatcheza ili tushinde maana najua ushindi utainua ari kwenye kikosi na kupelekea tufanye vizuri kwenye michezo inayofuata”.

(Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Etienne Ndayiragije (kulia) akiteta jambo na kocha wake msaidizi namba mbili, Selemani Matola (kushoto) wakati wanasimamia mazoezi ya Taifa Stars.)

Etienne amesema ari imeongezeka baada ya kocha msaidizi Selemani Matola kujiunga na kikosi hicho  baada ya kumaliza majukumu ya kuiongoza kikosi cha Simba kwenye michuano ya Mapinduzi viswani Zanzibar na Erasto Nyoni akijiunga na timu baada ya kumaliza matatizo ya kifamilia.

Ushiriki wa Taifa Stars kwenye michuano ya CHAN umekuja baada ya miaka takribani 11 tokea ushiriki wao mwaka 2009 michuano hiyo ulipoanzishwa na ndiyo msimu ambapo Zambia walishiriki kwa mara ya kwanza na kushika nafasi ya 3 ikiwa ndiyo ya juu zaidi kwa upande wao kwenye CHAN.

Huu utakuwa mchezo wa 18 wawili hao kukutana, kwenye michezo 8 ya mwisho ambayo Stars imekutana na Zambia kwenye michuano tofauti kukiwa na mchanganyiko wa wachezaji wao wakigeni kwenye vikosi vyao, Zambia imeshinda mara 4, sare 3 wakati Stars imeshinda mara 1 pekee.

Ili Taifa Stars iweke hai matumaini ya kufuzu hatua inayofuata ya robo fainali, inahitaji ipate ushindi michezo yote mitatu ya makundi watakayocheza au kuwa na matokeo yatakayomfany awe na alama nyingi kuliko wote kwenye kundi D au alama nyingi zitakazomfanya ashike wapili kwenye kundi.

Kwa upande wa kocha wa Zambia aliyewahi kuwa kocha wa Yanga na timu ya taifa ya Uganda, Milutin Sredojevic 'Micho' amesema kikosi chake kitimamu na tayari kuvaana na Taifa Stars kwenye michuano hiyo.

Baada ya mchezo huo, Stars itashuka dimbani tena tarehe 23 Januari 2021 kukipiga na Namibia na kumaliza na Guine tarehe 27 Januari 2021.

HABARI ZAIDI

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea