Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tarimba azipania Simba na Yanga, SportPesa Cup

Jumanne , 22nd Jan , 2019

Michuano ya SportPesa Super Cup mwaka 2019, inatarajia kuzinduliwa leo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam kwa michezo miwili kupigwa.

Abasi Tarimba

Mchezo wa kwanza wa leo utakuwa ni kati ya Singida United na Bandari ya Kenya, majira ya saa 8:00 mchana huku Yanga ikiwakaribisha Kariobang Sharks ya hukohuko Kenya huku katika mchezo wa pili wa saa 10:00 jioni.

Kuelekea ufunguzi wa michuano hiyo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa SportPesa nchini, Abbas Tarimba, amevitaka klabu za Simba na Yanga kutumia vikosi vya kwanza ili kuepusha aibu ambayo imekuwa zikiionesha katika misimu miwili iliyopita.

"Imekuwa ni utamaduni wetu, Samahani nitatumia neno 'kudharau' haya mashindano, awamu hii hatutaki utani, tunataka kombe libaki nyumbani kwa maana kila siku limekuwa likienda nchi jirani. Tunavitaka vilabu vyote vya hapa nyumbani kuhakikisha vinafanya vizuri", amesema Tarimba.

"Nilivyokuwa naingia hapa nilikutana na kocha wa Yanga, nikamsisitiza kuwa hatutaki utani katika mashindano ya mwaka huu", ameongeza.

Awali, michuano hii ilikuwa ikifanyika mwezi Juni baada ya ligi kumalizika lakini Tarimba amesema kuwa imekuwa ikilalamikiwa na vilabu hasa vya Tanzania kuwa inapofika mwishoni mwa msimu, wachezaji wengi mikataba yao huwa inamalizika kwahiyo kukosa fursa ya kushiriki. 

Pia ameitaja sababu nyingine kuwa ni klabu hizo kutokuwa na muda mrefu wa maandalizi kutokana na ligi kumalizika, tofauti na timu za Kenya ambazo katika kipindi hicho ligi yao inakuwa inaendelea.

Mshindi wa michuano hiyo atajinyakulia kitita cha Dola za Kimarekani 30,000 ambazo ni takribani shilingi milioni 65 za Kitanzania, huku mshindi wa pili akijinyakulia Dola 10,000, wa tatu atapata Dola 7,500 na mshindi wa nne atapata Dola 5,000.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi