Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ten Hag amtaka Ronaldo kujiimarisha kwanza

Alhamisi , 4th Aug , 2022

Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag amesema Cristiano Ronaldo anaweza kufaa katika aina yake ya uchezaji lakini atahitaji kujiimarisha kwanza kabla ya kupata nafasi ya kuthibitisha kuwa anastahili nafasi katika kikosi cha kwanza.

Kocha Erik Ten Hag akimwelekeza jambo Ronaldo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Rayo Vallecano jumapili iliyopita.

Ronaldo hakuwepo katika kikosi cha United kwenye ziara ya maandalizi ya msimu mpya nchini Thailand na Australia, na pia alikosekana katika mchezo wa kirafiki waliofungwa goli 1 kwa 0 dhidi ya Atletico Madrid, lakini alicheza dakika 45 za kipindi cha kwanza katika mchezo dhidi ya Rayo Vallecano uliomalizika kwa sare ya goli 1 kwa 1 katika dimba la Old Trafford Jumapili iliyopita.

Ten Hag aliongeza kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno anaweza kufaa katika mfumo wake wa jinsi anavyotaka United icheze ila kwanza inabidi ajiimarishe kimwili na aonyeshe kwamba anaweza kutimiza majukumu ipasavyo.

Mustakabali wa Ronaldo ndani ya United umekuwa wa hali ya sintofahamu baada ya vyombo vya habari vya Uingereza kuripoti kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliomba kuondoka klabuni hapo ili acheze ligi ya mabingwa barani Ulaya.

United ambayo itacheza ligi ya Europa msimu huu, wataanza kinyang’anyiro cha ligi kuu ya Uingereza siku ya Jumapili dhidi ya Brighton & Hove Albion.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke